30/05/2022
Mapishi ya Sambusa Za Nyama
Mahitaji
½ kilo Nyama ya iliyosagwa
kijiko 1 kikubwa cha chakula cha Pilipili manga
▪︎Vitunguu maji vinne
Kijiko kimoja cha chakula cha kitunguu Thomu na tangawizi iliyosagwa
Mafuta ya kupikia Kiasi
Vijiko vinne unga ngano au ute wa yai kwa kufungia sambusa
Kaki za sambusa (unaweza kununua zilizokuwa tayari zimeshakatwa kwa ajili ya sambusa au k**a utanunua zile sheet pana utazikata kwa inchi 4 upana wa ruler yaani upate mistari 3
Maelekezo
Kausha nyama ya kusaga kwa kiyunguu swaumu (thomu) na tangawizi pamoja na chumvi mpaka ikauke vizuri Iwache ipoe.
Kata kata majani ya kotmiri weka upande Kata kata upate vipande vidogo vidogo(chop) vya vitunguu maji.
Zikate pili pili zako slice za mviringo vidogo vidogo.
Wakati ukimaliza matayarisho haya na nyama yako itakuwa ishapoa kabisa hapo ndio utachanganya,bizari nzima pamoja na pilipili manga pamoja na vitu vyote ulivyokwisha vitayarisha
Koroga unga ndani ya kibakuli au ute wa yai
Weka kaki kwa mfungo wa triangle yaani pembe tatu k**a kofia na
weka mchanganyiko wa nyama yako kiasi na uanze kuzifunga sambusa zako na ukifika mwisho hapo ndipo upake unga wako kwa ajili ya kuifunga isifunguke wakati wa kuchoma, pendelea kutumia kaki 2 kwa kila sambusa moja.
Kuchoma kwake ikiwa unazifanya na kuzichovya hapo hapo mafuta lazima yawe baridi (ninakusudia uweke mafuta na uzitie sambusa kabla hayajapata moto).
Na ikiwa uliziweka kwenye friji zikaganda basi unatakiwa uzichome kwa mafuta ya moto
Like, Comment uliza ikiwa hujaelewa kisha share na wenzako