Alochick - alome chickens

Alochick - alome chickens karibu tupeane elimu ya ufugaji wa kuku kibiashara wakati wa kungojea ajira umepita changamkia fursa sasa kujiepusha na umaskini wa kujitakia

CHICKEN BREEDS1. ARAUCANAThe Araucana trait of laying blue or greenish eggs has persisted and now breeders are attemptin...
09/10/2023

CHICKEN BREEDS

1. ARAUCANA
The Araucana trait of laying blue or greenish eggs has persisted and now breeders are attempting to standardize the physical makeup of the population and gain them recognition as a breed. Some of the Araucanas were rumpless and possessed some interesting ear tufts. In the future, these fowls will likely be developed into an interesting breed with both economic and ornamental attributes.

JINSI YA KUTENGENEZA CHAKULA CHA KUKU NYUMBANI KWAKO ~ GROWER MASH ( WIKI YA 9 - WIKI YA 18)Chakula bora cha kuku ni kil...
13/11/2020

JINSI YA KUTENGENEZA CHAKULA CHA KUKU NYUMBANI KWAKO ~ GROWER MASH ( WIKI YA 9 - WIKI YA 18)

Chakula bora cha kuku ni kile kinachomwezesha kuku kukua vizuri na kwa haraka, kuwa na afya bora, na kutaga mayai mengi.

Uwingi na ubora wa lishe ya kuku unaweza kuainishwa katika makundi 5 ya vyakula k**a ifuatavyo:

1. Vyakula vya kutia mwili nguvu
2. Vyakula vya kujenga mwili
3. Vyakula vya kuimarisha mifupa
4. Vyakula vya kulinda mwili, na
5. Maji.

Ufuatao ni mfano wa Kutengeneza chakula cha Kuku Kilo 100.

yaliyobarazwa au mtama au uwele 25
za mtama au mahindi au uwele 44
ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17
wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 3.25
au mabaki ya samaki (fish meal) 10
ya jikoni 0.25
(Broiler premix) 0.5.
JUMLA = 100Kg

Karibu "Alochik" wafugaji wa Kuku. Tupo Songwe-Tunduma. ☎️0746090774

JINSI YA KUTENGENEZA CHAKULA CHA KUKU NYUMBANI KWAKO ~ CHICK MASH    ( WIKI YA 1 - WIKI YA 8)Mambo muhimu ya kuzingatia ...
13/11/2020

JINSI YA KUTENGENEZA CHAKULA CHA KUKU NYUMBANI KWAKO ~ CHICK MASH ( WIKI YA 1 - WIKI YA 8)

Mambo muhimu ya kuzingatia katika kuandaa chakula
cha kuku

• Upatikanaji wa malighafi k**a:- Mahindi mtama, pumba, nk. Kutegemeana
na kinachopatikana katika eneo husika.
• Uchaguzi wa malighafi utategemea uwezo wa mfugaji.
• Utengenezaji wa chakula unategemea rika la kuku unaowatengenezea.
• Kiasi au uwingi wa chakula kitakachotengenezwa kitategemea uwezo wa
mfugaji kifedha.
• Mali ghafi zinazotumika kutengenezea chakula ziwe zimekauka vizuri ili
kuepuka uwezekano wa kuota ukungu ambao ni hatari kwa afya ya kuku.
• Hata k**a mali ghafi ni kavu ikaguliwe kuhakikisha kwamba haina ukungu
na iwe haijaoza.

wa nafaka k**a mahindi au mtama Kilo 40
za mtama, mahindi, uwele Kilo 27
ya, alizeti, , ufuta karanga au pamba n.k Kilo 20
wa mifupa au chokaa ya kuku Kio 2.25
au mabaki ya samaki Kilo 10
0.25
(Premix) 0.5
Jumla Kilo 100

Karibu "Alochik" wafugaji wa Kuku . Tupo Sonnwe-Tunduma. Kwa mahitaji mbalimbali ya Vifaranga na Kuku, Ushauri ama swali 0746090774(Call/Whatsaap/Text/Telegram)

KOSA KUBWA LINALOFANYWA NA WAFUGAJI WENGI BILA KUJUA.Masomo mengi ya utoaji chanjo kwa kuku yamekuwa yakieleza ratiba za...
13/11/2020

KOSA KUBWA LINALOFANYWA NA WAFUGAJI WENGI BILA KUJUA.

Masomo mengi ya utoaji chanjo kwa kuku yamekuwa yakieleza ratiba za utoaji chanjo bila ya kusisitiza jambo muhimu zaidi ambalo ni matumizi sahihi ya chanjo husika.
Hapa nazungumzia chanjo zinazochanganywa na Maji. (Oral Live Vaccines). eg. Newcastle, Gumboro (IBD) etc.

Kutokana aina za chanjo tajwa hapo juu zinahitajika kuchanganywa na maji ndipo uwapatie kuku kwa muda usiozidi masaa mawili, basi wafugaji wengi hatufahamu kuwa si Kila maji unaweza kuchanganya na chanjo hizo.

Hapa nazungumzia maji ya Bombani. Ikumbukwe kuwa maji mengi ya bombani hasa kipindi hiki huwa yanakuwa treated/yanatibiwa/yanawekwa dawa ili kuhakikisha mtumiaji anapata /kunywa maji safi na salama.

Hivyo utakapoyatumia wewe mfugaji kwa ajili ya kuchanganya na chanjo itapelekea chanjo yako kutokuwa kamilifu kiutendaji kazi (inefficiency) kutokana na maji uliyotumia tayari yana dawa ya kutakasa maji haswa Chlorine ambayo inakinzana na utendaji kazi wa chanjo uliyochanganya.

In short ni kwamba, pendelea kutumia maji safi ya Kisima, Mvua ama maji yasiyokuwa na chlorine/ambayo hayajaekwa dawa.

Ila sasa, kutokana na maeneo mengi ni ngumu kupata maji hayo.! itakupasa utumie dawa za Dechlorination uchanganye na maji ya bomba kwanza ili kutoa chlorine iliyochanganywa kwenye maji hayo ndipo uyatumie kuchanganya na chanjo uliyoiandaa.

Baadhi ya wafugaji huchemsha maji yao kabla ya kuyatumia kwa ajili ya chanjo lakini niwashauri tu wafugaji wenzangu kuwa, ukichemsha maji huondoi chorine kwenye maji labda kwa kiasi fulani tuu, ila kwa uhakika zaidi itakubidi uyachanganye maji hayo na maziwa ya Unga (Milk powder). Ingredients za milk powder husaidia kuondoa chlorine kwenye maji k**a njia m,badala ya kutumia dawa special kwa ajili ya dechlorination.

Niishie hapo kwa leo, ila k**a una swali ama ushauri tucheki kupitia namba zetu. 0783-554005 (Call/Whatsapp/Txt)

Tupo Mbeya Tunduma
0746090774

UGONJWA WA KIDERI (NEW CASTLE DISEASE)-ugonjwa wa kuku unasababishwa na virus aina ya paramyxovirus-unafanya kuku kukosa...
13/03/2020

UGONJWA WA KIDERI (NEW CASTLE DISEASE)

-ugonjwa wa kuku unasababishwa na virus aina ya paramyxovirus
-unafanya kuku kukosa hamu ya kula na kunyongonyea
-kuku wanapata vikohozi na kushindwa.kupumua vizuri
-kuku wanaparalaizi na kupindisha shingo kwa nyuma
-kuku wana harisha kinyesi cha kijani k**a maji maji

Ugonjwa unawapata sana vifaranga na wanakufa kwa wingi (siku 1 mpka 7)

*MUHIMU*
Ugonjwa huu unazuilika kwa CHANJO wanayopewa kuku siku saba za kwanza baada ya kuzaliwa

Kuku waliogua tayari huu ugonjwa wanaushiriwa kupewa dawa za kupunguza maambukizi zaidi na kutengwa na walio wazima mpka watakapo pata nafuu na kupewaa chanjo upya

Kwa maelezo zaidi tupigie
0746090774

14/01/2020

UGONJWA WA KUHARA DAMU KWA KUKU. (COCCIDIOSIS)

      Coccidiosis ni ugonjwa wa kuhara damu unaosababishwa na vijidudu wajulikanao kwa jina la "Protozoa". Wadudu hawa hushambulia sehemu mbalimbali za utumbo wa kuku.

MAZINGIRA YANAYO SABABISHA COCCIDIOSIS.
      Unyevu kwenye matandazo/maranda (litter material).
      Kutobadilisha matandazo/maranda kwa muda mrefu.
      Kuhamishia vifaranga kwenye sehemu waliyokuwa wanakaa kuku wakubwa bila kufanya usafi.
      
      DALILI ZA COCCIDIOSIS.

      Kuharisha; kwanza kinyesi huanza kuwa laini, pili hubadilika rangi kuwa kijivu na baadaye mchanganyiko wa damu na kuonekana k**a kahawia au rangi ya udongo au brauni.
      Manyoya yasiyo na mpangilio na yaliyosinyaa, kuku hapendezi na hukunja mabawa k**a amevaa koti.  Kuku kupauka(paleness), hususani kwenye viremba(comb/wattle) na miguuni kutokana na kukosa damu.

      Kukua polepole(poor growth).
      Kukosa hamu ya kula.
      Vifo vingi hasa vifaranga.
      Kupungua uzito.
      Kushusha utagaji.

      NAMNA YA KUZUIA COCCIDIOSIS.

      Epuka unyevu kwenye maranda(litter material) na banda kwa ujumla.
      Tumia dawa za kukinga ugonjwa (coccidiostats).
      Badilisha maranda kabla ya kuingiza vifaranga au kuku wapya.

      JINSI YA KUTIBU COCCIDIOSIS. Tumia (i) Esb3 - Kwenye maji au (ii) Amprolium -Kwenye maji.

      MUHIMU
''Matibabu yote ni muhimu kutumia dawa ya vitamin (multivitamin) k**a nyongeza kwa muda wa siku tatu zinazoachana kwa ajili ya kuongeza hamu ya kula''''''

UKIITAJI KITABU CHA UFUGAJI BORA WA KUKU
HARDCOPY SH 10000
SOFTCOPY SH 5000 UNATUMIWA KWA EMAIL AU WHATSAPP

TUNAPATIKANA MBEYA
BY
ALOCHICK
0746090774

07/01/2020

Je umeshaaanzisha mradi wako wa Kuku, Lakini hauna usaidizi wa Daktari anayekutembelea angalau Mara 2 kwa Mwezi,

Ili kukupatia Ushauri wa Mara kwa Mara kuhusu Namna ya Kuboresha mradi wako?

Ili uepukane na hasara mbalimbali zitokanazo na Magonjwa ya Kuku,

Ulishaji mbaya,

Matumizi mabaya ya Dawa au Chanjo.

Ili uweze Kuongeza KIPATO CHAKO!

Leo KPTL tumekuletea Huduma Bora ya Usimamizi wa mashamba (Farm Management)

Ambapo Daktari wetu atakutembelea mara 2 kwa Mwezi na kukupatia usaidizi wa mara kwa mara

Ili uboreshe mradi wako na uweze KUONGEZA KIPATO CHAKO.

K**a unahitaji huduma hii ya Usimamizi wa Mashamba (Farm Management)

Wasiliana nasi kupitia
0752 672 181

Karibu Ofisini kwetu

Dar, Kijitonyama Bamaga.

27/12/2019

MAZOEA YANAYOWAGHARIMU WAFUGAJI WA KUKU

Kuna baadhi ya wafugaji huwa wanafuga kwa kutegemea uzoefu walionao katika ufugaji bila ya kujali kuwa kuna mabadiliko kila siku katika sekta ya mifugo, wengi wao huwa wanatatua kesi mbalimbali zinazotokea katika ufugaji kwa kutumia uzoefu hali ambayo inawasababishia kupata hasara kubwa isiyo ya lazima. Yafuatayo ni baadhi ya mazoea yanayowagharimu wafugaji:-

1. KUINGIZA VIFARANGA BILA MAANDALIZI SAHIHI

Wengi wa wafugaji huwa wanaingiza vifaranga pasipo kufuata utaratibu wa kitaalam katika kuandaa banda pamoja na maandalizi ya kupokea vifaranga. Na k**a atabahatika kufanya usafi basi atafanya juujuu tu hali ambayo inasababisha banda kuhifadhi vimelea vingi vya magonjwa na kupelekea kuku kuugua na kufa kuanzia wanaingia hadi kufikia kuuzwa, na hatimaye mfugaji hupata hasara kwani hutumia pesa nyingi kwenye madawa kwa kutibu na pesa nyingi kwenye chakula kwa kuchelewa kukua kutokana na kuumwa.

2. KULISHA BILA KUFUATA MAELEKEZO SAHIHI
Kila aina ya kuku wanautaratibu wa ulishwaji chakula, utaratibu ambao ukikiukwa huwezi kupata matokeo mazuri ya mifugo yako, ila wafugaji wengi huwa wanalisha kwa utaratibu usio sahihi ambao wao wanadhani kwamba ndio wataongeza
uzalishaji wa mayai au watakuwa haraka kwa upande wa kuku wa nyama, na kuna wengine wanadiriki kutumia chakula aina moja mwanzo mwisho, yaan anaweza kutumia chakula cha
vifaranga wa nyama (SUPER STARTER) kuanzia mwanzo hadi anauza kuku bila kufaham kwamba kila aina ya chakula ina kazi yake katika kila hatua ya umri. Lakini pia bila kujali kwamba analisha kwa gharama kubwa hali ambayo itampunguzia faida.

3. KUTIBU KWA DAWA AMBAYO SI CHAGUO KWA UGONJWA HUSIKA
K**a inavyofahamika kuwa wafugaji wa kuku wengi wamebarikiwa kwa kufaham majina mengi ya dawa za kuku, na kwa kutumia uzoefu walionao huwa wanatibu kuku wao magonjwa mbalimbali bila kupata maelekezo kutoka kwa Dokta au Mtaalam wa mifugo. Kwa kufanya hivyo hutumia dawa nyingi tofautitofauti kwa kutibu ugonjwa mmoja bila mafanikio na kupelekea ugonjwa kuwa sugu na idadi ya vifo kuongezeka siku hadi siku.

USHAURI:
Sio kila mfugaji mzoefu anaweza kuwa Daktari, ila kila Daktari anaweza kuwa mzoefu.

UKIITAJI KITABU CHA UFUGAJI WA KUKU WASILIANA NASI 0746090774

HARDCOPY SH 10000
SOFTCOPY SH 5000 UNATUMIWA KWA EMAIL AU WHATSAPP

BY
ALOME BROWN

[ KITINI BURE ] Ufugaji Bora Wa Kuku Wa Asili (Kuku wa Kienyeji)Bonyeza hapa Kukipata>> http://www.tfcg.org/wp-content/u...
22/12/2019

[ KITINI BURE ] Ufugaji Bora Wa Kuku Wa Asili (Kuku wa Kienyeji)

Bonyeza hapa Kukipata
>>http://www.tfcg.org/wp-content/uploads/2018/08/AVA-Improved-poultry-farming-training-materials-2017.pdf

Chanzo cha kitini hichi ni Tanzania Forest Conservation Group

Jumapili njema kwenu..

22/12/2019

Hatak**a Uko Busy, Basi Jitahidi Weekend Nenda Shamba Kaone Maendeleo Ya Mifugo Yako

Hasara nyingi zimetokana na wafugaji kutokuiangalia Miradi kwa Ukaribu

Epuka HASARA zitokanazo na Kutokuiangalia Miradi kwa UKARIBU

Kumbuka Umewekeza Fedha Yako, Usiache Ipotee Kirahisi

Inuka Nenda Shamba, Acha Kufuga Kwa Simu

10/03/2019

Address

Tunduma
Mbeya

Opening Hours

Monday 08:00 - 18:00
Tuesday 08:00 - 18:00
Wednesday 08:00 - 18:00
Thursday 08:00 - 18:00
Friday 08:00 - 18:00

Telephone

+255652241228

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Alochick - alome chickens posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Restaurant

Send a message to Alochick - alome chickens:

Share

Category