Domcity Farming Center

Domcity Farming Center kufuga kuku kibiashara unatakiwa uwe na vitu vifuayavyo
AVAILABILITY, COMMITMENT, PASSION, LOCATION AND RESOURCES. Ushauri
Tupigie/WhatsApp 0656626173

🤷 HELLO HELLO MKO POUWAAA....🙏...AMANI YA MOLA IWE JUU YENU...🙏
02/12/2024

🤷 HELLO HELLO MKO POUWAAA....

🙏...AMANI YA MOLA IWE JUU YENU...🙏

🤲Amani Ya Mola Iwe Juu Yenu...🤲🤔Watu Wengi Wanajiuliza Ni Kuku Gani Wanafaa Kufugwa Kibiashara...???😔Uwenda Wewe Unayeso...
04/04/2023

🤲Amani Ya Mola Iwe Juu Yenu...🤲

🤔Watu Wengi Wanajiuliza Ni Kuku Gani Wanafaa Kufugwa Kibiashara...???

😔Uwenda Wewe Unayesoma Post Hii Ni Miongoni Mwa Watu Wanaojiuliza Hilo Swali... Sasa Leo Nitawajibu Hili Swali Kwa Urefu Sana Naomba Utulivu Wako Ili Uweze Kunielewa...

👉Kwanza kabsa tunatambua hapa kwetu Tanzania kuku wanaofugwa ni k**a ifuatavyo
1️⃣Kuku wa nyama(Broilers)
2️⃣kuku wa mayai (Layer's)
3️⃣Kuku chotara(kroiler, sasso,tanbro n.k)
4️⃣kuku wa kienyeji

👍Nazani mpaka hapo tupo pamoja👍

😋Katika hizo aina za kuku ukiwauliza watu unapenda kitoweo Cha kuku gani asilimia kubwa watakujibu KUKU WA KIENYEJI🐓🐓🐓

😊Ni kweli KUKU WA KIENYEJI wanapendwa sana kuliko aina yoyote ya kuku kuanzia kwenye nyama mpaka mayai yake

😥Ila Mimi k**a DOMCITY FARMING CENTER sikushauri kufuga kuku wa kienyeji k**a kuku wa biashara...

🥳KWANINI SIKUSHAURI KUFUGA KUKU WA KIENYEJI K**A KUKU WA BIASHARA..???🥳

✍️Kuku wa kienyeji wanachukua mda mrefu sana kufikia uzito wa kitoweo ni kuanzia miezi 5-6 mpaka miezi 7

✍️Kuku wa kienyeji wanataga mayai machache sana kwa mwaka wastani wao wa kutaga ni mayai 60-70

🧐Kwahyo utalazimika kufuga kuku kwa mda mrefu uku ukiingia gharama za chakula ila faida yake ni ya kuchelewa halafu ni ndogo sana

🚨ANGALIZO
✍️Usipokua makini kwenye ufugaji wa kuku wa kienyeji unaweza jikuta unafuga kwa hasara bila wewe kujijua endapo hautafanya mahesabu ya chakula walichokula mpaka mda wa kuwauza

🔥SWALI KWAKO MSOMAJI...🔥
🤔Ushawahi kujiuliza kwanini Wafugaji wakubwa wanafuga aina hizi za kuku na sio kienyeji 👇👇👇

1️⃣KUKU WA MAYAI
2️⃣KUKU WA NYAMA(BROILERS)
3️⃣KUKU CHOTARA (sasso, tanbro, kroiler..)

😇Kwa jawabu la haraka haraka utasema Hawa Wafugaji wakubwa wanamitaji mkubwa ndio maana wanafuga aina hizo za kuku...

🤨Ni kweli ufugaji unahitaji mtaji ila sio lazima uwe na mtaji Mkubwa ndio ufuge kuku kibiashara

🤗Ushauri wangu kwako Ukitaka kufuga kuku kibiashara k**a unaweza Fuga KUKU WA MAYAI k**a hao hauwezi Fuga BROILERS k**a hao hauwezi Fuga CHOTARA ikishindikana kabsa basi Fuga KUKU WA KIENYEJI...

👉K**a unaswali uliza...???

NB:MAONI YA YANGU SIO SHERIA

🇹🇿 MBARIKIWE SANA
🇹🇿 DOMCITY FARMING CENTER
🇹🇿04 APRIL 2023

Amani Ya Mola Iwe Juu Yenu...🎯K**a Unapenda Kuwa Mfugaji Mkubwa Hapa Tanzania Anza Leo Kuwaza Tofauti Na Wafugaji Waliok...
17/03/2023

Amani Ya Mola Iwe Juu Yenu...

🎯K**a Unapenda Kuwa Mfugaji Mkubwa Hapa Tanzania Anza Leo Kuwaza Tofauti Na Wafugaji Waliokutangulia...

✍️Sina Maana Tusijifunze Kwa Waliotangulia Hapana Ila Inatubidi Tuwaze Tofautii Ili Kuleta Ushindani Sokoni...

✍️Twende Kwenye Mada Husika Ili Tupate Kuelewana Aya Twende Pamoja Sasa...

👉Ufugaji Ni Biashara K**a Biashara Zingine Ubunifu Ni Muhimu Sana Na Unaweza Ukakuletea Mafanikio Ya Kushangaza Katika Safari Yako Ya Ufugaji

NOTE:::MFANO WA UBUNIFU UNAOWEZA KUUFANYA NA UKAKULETEA MAFANIKIO MAKUBWA NI

1.KUTAFUTA MBEGU ZA KIENYEJI WENYE SIFA ZA KUTAGA MAYAI MENGI NA UKAWA UNAFANYA BIASHARA YA KUUZA MAYAI PURE YA KIENYEJI NA K**A TUNAVYOJUA SOKONI HAYO MAYAI HAYANA MPINZANI..

2.UNAWEZA UKAFANYA ZOEZI LA KUTAFUTA MBEGU KUBWA ZA KUKU WA KIENYEJI MFANO UKAPATA MATETEA WAKUBWA KUTOKA SINGIDA NA MAJOGOO WAKUBWA KUTOKA MWANZA AU KAHAMA AU TABORA UKAFUGA NA KUZALISHA VIFARANGA WA TOFAUTI NA WAFUGAJI WENGINE.. WATU WATAPENDA NA PIA UTAFANYA BIASHARA YA KUUZA VIFARANGA AU KUKU WAKUBWA AU MAYAI YAO N.K

Hiyo Ni Baadhi Tu Ya Mifano Ya Kufanya Ufugaji Tofauti Na Wafugaji Wengine Na Ukajikuta Hauna Ushindani Sokoni Kabsa Sio Lazima Utumie Hiyo Mifano Unaweza Buni Wewe Kwa Jinsi Unavyowaza Nje Ya Box..

2NOTE:::FANYA UFUGAJI WAKO KATIKA HALI YA UBORA ATAK**A UNAKUKU WACHACHE...

✍️K**A UNATAMANI KUWA MFUGAJI MKUBWA HAPA TANZANIA FANYA VITU VYAKO KWA UBORA HII ITAKUFANYA UVUTE WATEJA WENGI SANA KWASABABU YA UBORA WA KUKU WAKO...

✍️ TUMEKUA NA KAWAIDA YA KUDHARAU... MFANO UKIFUGA KUKU WACHACHE UNAWAFUGA KIKAWAIDA KWASABABU YA UCHACHE WAO NA KUPELEKEA KUZALISHA KUKU WASIO NA UBORA MWISHOWE UNAPOTEZA WATEJA...

🪀ZINGATIA VITU VIFUATAVYO ILI UFUGE KUKU KATIKA UBORA
1.BANDA BORA
2.MBEGU BORA
3.CHAKULA BORA
4.USIMAMIZI BORA

✍️HIVYO NI BAADHI YA VITU AMBAVYO UKIVIFANYA VINAWEZA KUKULETEA MATOKEO CHANYA SANA KWENYE SAFARI YAKO YA MAFANIKIO YA UFUGAJI

JE...? WEWE NI KITU GANI UNASHAURI WATU WAFANYE ILI WAFANIKIWE ZAIDI KWENYE HII SECTOR YA UFUGAJI...???

🇹🇿 MBARIKIWE SANA 🙏
🇹🇿 DOMCITY FARMING CENTER
🇹🇿17 MARCH 2023

Amani Ya Mola Iwe Juu YenuKwanini Tunaghairisha Kuanza Ufugaji...(SEHEMU YA PILI)🗣️Tuseme kwa pamoja Nitaanza kidogo kid...
12/03/2023

Amani Ya Mola Iwe Juu Yenu

Kwanini Tunaghairisha Kuanza Ufugaji...(SEHEMU YA PILI)

🗣️Tuseme kwa pamoja Nitaanza kidogo kidogo ili nitimize malengo yangu...Hayaa Turudie tenaaa

🗣️Nitaanza kidogo kidogo ili nitimize malengo yangu...

🚨Kuna Mda Tumekua Tukichelewa Kuchukua Maamuzi Ya Kuanza Ufugaji kwasababu Ya Mihemko Ya Kutaka Kuanza Kufuga Kwa Ukubwa Ulio Nje Ya Uwezo Wetu...

✍️Tuelewane Kidogo Kuanza Ufugaji Na Mtaji Mkubwa Sio Vibaya Ila Ni Vizuri Zaidi Kuanza Na Ufugaji Mdogo Atak**a Unamtaji Mkubwa...

🛑Tumekua tukijipa pressure kubwa kwasababu ya Kutaka Kuanza hatua kubwa...

Swali..???
🤔Kwanini ujipe pressure kwa kuanza Ufugaji mkubwa wakati unaweza ukaanza na ufugaji wa mtaji wa kawaida halafu ukakufikisha uko unakotaka ufike...???

🥳KWANINI NASHAURI WATU WAANZE NA UFUGAJI WA KAWAIDA(MDOGO)

✍️ Kwanza Hii itakusaidia uachane na tabia ya kughairisha,,,, nitaanza kesho... sijui mwezi ujao... sijui mwaka ujao... kwasababu watu wengi wameghairisha kuanza ufugaji kwakulazimisha kutafuta mtaji mkubwa ili aanze ufugaji mkubwa jambo ambalo sio sahihi...❌

✍️Pia kuanza na Ufugaji Mdogo itakusaidia kukupa nguvu kwasababu utajifunza mengi kupitia huo ufugaji mfano soko lipoje...wateja wanahitaji nini... Jinsi ya kufata utaratibu wa chanjo... ni mda gani sahihi wa kununua vifaranga kwaajili ya kuja kuwakuza na kuwauza kwa siku sijazo... N.k kuliko kuanza na Mtaji Mkubwa ambao ukipata changamoto inaweza sababisha usifuge tena..😥

✍️Na pia itakusaidia kufuga bila pressure yoyote chukua Dk moja tu jaribu kuwaza aliyeanza ufugaji mkubwa na aliyeanza na ufugaji mdogo nani atakua kwenye pressure kubwa ya kuwaza..🥳

🎯Maneno yangu sio Sheria ila k**a wewe ni miongoni mwa watu wanaochelewa kuchukua Maamuzi ya kufuga kwasababu ya Kutaka Kuanza kwa Ukubwa my friend unajichelewesha kuanza safari ya kutimiza ndoto zako...

🎉🎉Tuanze kidogo kidogo itatupa hamasa,itatupa ujasiri,tutajifunza mengi, na pia itatupa uzoefu wa kufanya kwa Ukubwa Zaidi...

😘NA KIKUBWA ZAIDI TUTATIBU TABIA YA KUGHAIRISHA KWASABABU KUANZA KIDOGO HAKUNA STRESS SANA🥰

🇹🇿 MBARIKIWE SANA 🙏
🇹🇿 DOMCITY FARMING CENTER
🇹🇿12 MAR 23

Amani Ya Mola Iwe Juu Yenu🤔Kwanini Unashindwa Kuchukua Maamuzi Ya Kuanza Ufugaji..???🎉Mada ya Leo itahusika zaidi kuzung...
12/03/2023

Amani Ya Mola Iwe Juu Yenu

🤔Kwanini Unashindwa Kuchukua Maamuzi Ya Kuanza Ufugaji..???

🎉Mada ya Leo itahusika zaidi kuzungumza na wewe unayesoma hii post....

🥵Kwanini...??? kila sekunde...kila dakika...kila saa...kila siku...kila wiki...kila mwezi...kila mwaka umekua mtu wa kughairisha maamuzi ya kuanza ufugaji...???

🪀Uwenda unaghairisha kufanya maamuzi kwasababu 👇👇👇
✍️Ni tabia yako ya uvivu inakufanya uwe hivyo
✍️Unawaza sana changamoto zilizopo kwenye icho kitu unachotaka kukifanya
✍️Umesikia maneno mengi ya kukatisha tamaa kuhusu icho kitu unachotaka kukifanya

🎯Kabla ya yote inabidi ujue ni kitu gani kimejificha nyuma ya hiyo tabia ya kughairisha maamuzi yako ambayo ni sahihi ukiyatazama...

🎯Jambo lenyewe ni UOGA na akili yako inakuambia njia nzuri ya kukimbia UOGA ni kutokufanya chochote na ndio maana mpaka Leo haujachukua maamuzi yoyote na siku zinazidi kwenda na miaka inazidi kukatika..😔😔😔

🎯Uwenda hii tabia unaishi nayo bila kujijua Au umeshindwa kujua ni hatua gani za kupitia hili uachane na hiyo hali... Basi Leo nitakupa majibu ya jinsi ya kuepukana na hiyo hali na uchukue maamuzi Leo Leo...

✍️Kwanza jikumbushe mwenyewe hasara za kutotimiza ndoto zako kwa wakati..Itakusababishia uje utimize malengo yako ukiwa umechelewa na umri umeenda na hapo utakua na majuto yasiyo na tija..Pia Utakuja kujilaumu kwanini haujafanya kitu ambacho ulikua unaweza kukifanya na wakati huo hauna nafasi ya kufanya tena

✍️Acha kufatisha akili yako inavyotaka..Akili yako itakuambia vitu vifuatavyo
👉Nimechoka...
👉 Nitafanya kesho...
👉Sahivi nikianza sitafanya vizuri ngoja nitafute mtaji mkubwa ndio nianze...
👉Kwasasa sio muhimu nitaanza siku yoyote tu...
👉Nataka kupumzika kwasasa mda ukifika nitaanza..n.k

🚨Hautakiwi kusikiliza akili yako inatakaje kwasababu itakufanya uwe mtumwa wa akili...

🚨Na ukishakua mtumwa wa akili yako bhasi utakupambana na maisha yafuatayo
😥Hautaishi maisha unayoyataka au kuyatamani siku moja uje kuyaishi
😥Hautatimiza ndoto zako
😥Na k**a utakuja kutimiza bhasi kwa kuchelewa...

Je...? Wewe msomaji ni kitu gani kinakufanya Ushindwe kuanza ufugaji...??

🇹🇿MBARIKIWE SANA🙏
🇹🇿DOMCITY FARMING CENTER
🇹🇿12 MAR 23

🙏Amani Ya Mola Iwe Juu yenu🙏🚨Taharifa Kwa Wafugaji Wa kuku...🚨✍️JE...??? NI CHANGAMOTO GANI UNAYOKUMBANA NAYO KWENYE UFU...
04/03/2023

🙏Amani Ya Mola Iwe Juu yenu🙏

🚨Taharifa Kwa Wafugaji Wa kuku...🚨

✍️JE...??? NI CHANGAMOTO GANI UNAYOKUMBANA NAYO KWENYE UFUGAJI WA KUKU KWASASA....???

AMANI YA MOLA IWE JUU YENUSEHEMU YA TATU⛑️⛑️MAKOSA TUNAYOFANYA WAKATI WA KUANZISHA MRADI WA UFUGAJI WA KUKU ⛑️⛑️3️⃣KUAMI...
19/10/2022

AMANI YA MOLA IWE JUU YENU

SEHEMU YA TATU

⛑️⛑️MAKOSA TUNAYOFANYA WAKATI WA KUANZISHA MRADI WA UFUGAJI WA KUKU ⛑️⛑️

3️⃣KUAMINI MTAJI NDIO KILA KITU KWENYE UFUGAJI KULIKO MAARIFA

🗣️Ukitaka post yako isipate LIKES na COMMENTS nyingi wakumbushe wafugaji umuhimu wa kutafuta maarifa ya ufugaji..

🗣️Hili tatizo alitakuja kuisha kwasababu wafugaji wengi wanapenda kuona mafanikio na sio kujua mchakato wa mafanikio

🗣️Kwa kuwakumbusha tu hao unaowaona wamefanikiwa kwenye ufugaji walitenga mda wao kujifunza kwahyo k**a unatamani kuwa k**a wao usione uvivu kujifunza🤝🤝🤝

📩Turudi kwenye mada yetu husika miongoni mwa makosa tunayofanya wakati wa kuanzisha mradi wa ufugaji wa kuku ni kuamini mtaji ndio kila kitu kwenye ufugaji kuliko MAARIFA..

👉Twende kwa mfano ili tuelewane vizuri

🚥🚦JE..?? NI WAFUGAJI WANGAPI WAMEKURUPUKA KUANZA UFUGAJI KISA TU KAPATA MKOPO AU KAPATA PESA..??

🚦🚥JE...?? NI WAFUGAJI WANGAPI WAMEKURUPUKA KUANZA UFUGAJI KISA TU ALISHAWISHIWA NA MTU KUWA KUKU WANALIPA AU ALIIGA KWA MTU BAADA YA KUONA KAFANIKIWA..??

🔔MARA NYINGI WATU WANAPOTEZA PESA ZAO KWA KUANZISHA MRADI BILA KUWA NA MAARIFA YA UFUGAJI

🔔HATUKATAI MTU ANAWEZA KUANZA THEN AKAJIFUNZA KADRI SIKU ZINAVYOKWENDA ILA HII MARA NYINGI HUWA NI HATARI(RISK) KWASABABU UTAFANYA MAKOSA AMBAYO YANAWEZA KUKUGHARIMU KUPOTEZA PESA YAKO

🔔HIVI UNAAMINI WATU WENGI WAMEANZISHA MRADI WA KUKU KISA WANAMTAJI ILA HAWANA MAARIFA YA UFUGAJI NA IMEWAPELEKEA MRADI KUFA NDIO ANAPATA UFAHAMU WA KWANINI KAFELI...??

🔔TUSIPOTEZE MDA NA PESA KWA KUKURUPUKA TUJITAHIDI KUTAFUTA MAARIFA NA K**A UNAONA MTAJI NINAO NA HAUNA MAARIFA YA UFUGAJI TAFUTA MTU WA KUKUONGOZA HII ITAKUSAIDIA KUPUNGUZA MAKOSA AMBAYO YANGEKUGHARIMU KUPOTEZA PESA ZAKO...

🔔KUKURUPUKA KUANZISHA MRADI KISA UNAMTAJI WAKATI ELIMU YA UFUGAJI HAUNA MADHARA YAKE NI K**A IFUATAVYO..👇👇👇

🛑KUPATA VIFO VINGI VYA VIFARANGA MFANO ULINUNUA VIFARANGA 500 WANAKUJA KUPONA 200 AU 100

🚨KUKU KUKUMBWA NA MAGONJWA MFULULIZO

👺MRADI KUWA NA GHARAMA NYINGI KULIKO KAWAIDA N.K

👏MUHIMU TUTUNZE MITAJI YETU KWA KUTAFUTA ELIMU YA UFUGAJI..

SOMO LINAENDELEA..

🇹🇿 MBARIKIWE SANA 🙏
🇹🇿 DOMCITY FARMING CENTER
🇹🇿19 OCT 2022

AMANI YA MOLA IWE JUU YENUSEHEMU YA PILI⛑️⛑️MAKOSA TUNAYOFANYA WAKATI WA KUANZISHA MRADI WA UFUGAJI WA KUKU ⛑️⛑️2️⃣KUTOK...
17/10/2022

AMANI YA MOLA IWE JUU YENU

SEHEMU YA PILI

⛑️⛑️MAKOSA TUNAYOFANYA WAKATI WA KUANZISHA MRADI WA UFUGAJI WA KUKU ⛑️⛑️

2️⃣KUTOKUJUA MBEGU SAHIHI YA KUFUGA KULINGANA NA MALENGO YAKO

👉Hii sehemu naomba weka utulivu wa kutosha ili twende sawa kwasababu ni kipengele muhimu sana kwa mfugaji anayefuga kuku kibiashara

👉Kuna aina kuu mbili za kuku ambazo ni
1.INDIGENOUS CHICKEN (kuku wa asili)

2.EXOTIC CHICKEN (Broilers, layers na chotara)

👉Wewe k**a mfugaji inabidi ujue unataka kufuga aina gani ya kuku kulingana na biashara unayotaka kuifanya

✍️Tunaposema ufugaji wa kuku kibiashara huwa tunategemea kuuza vitu vifuatavyo
🐣Kuuza vifaranga 🐣
🥚Kuuza mayai🥚
🐓Kuuza kuku🐓

✍️Kwakua malengo yetu ni hayo muhimu kujua kila aina ya kuku na sifa zao ili iwe rahisi kufanya uchaguzi wa mbegu kulingana na biashara unayotaka kuifanya

🐓KUKU WA ASILI🐓
✍️Hawa ni kuku ambao huwa tunawaita kuku wa kienyeji na sifa za kuku wa kienyeji ni k**a ifuatavyo👇👇

📩Wanataga mayai 60-70 kwa mwaka

📩Wanachukua miezi 5-6 kuwa kuku wakubwa na kufaa kwa kitoweo

📩Nyama yao inaradha tamu kuliko aina nyingine za kuku

📩Wanatamia mayai baada ya kutaga

📩Wanauwezo wa kujitafutia chakula wenyewe

🐔KUKU WA KISASA🐔
✍️Hawa ni kuku ambao wamefanyiwa maboresho na wanasifa tofauti na kuku wa asili yaani kuku wa kienyeji

✍️Kuku wa kisasa ni broilers, chotara na layers (kuku wa mayai) sifa zao ni👇👇

📩Wanakua kwa haraka sana ndani ya mda mfupi anafaa kwa kitoweo

🐤 Mfano broilers ndani ya wiki 4 sawa na mwezi mmoja anakua tayari kwa kitoweo

🐤Chotara ndani ya wiki 8-12 wanakua tayari kwa kitoweo ambapo ni sawa na miezi 2 mpaka 3

📩Kuku wa kisasa Wanauwezo wa kutaga mayai 200-300 kwa mwaka

🐤Mfano chotara wanaweza kutaga mayai 200-250 kwa mwaka

🐤 Layers (kuku wa mayai) Wanauwezo wa kutaga mayai 200-300

📩Kuku wa kisasa hawana uwezo wa kuatamia kwahiyo mayai yao yanatotoleshwa kwa kutumia mashine za kutotoleshea(INCUBATOR)

📩Kuku wa kisasa k**a vile broilers hawana uwezo wa kujitafutia chakula ila chotara k**a vile Sasso, kroiler n.k wao Wanauwezo wa kujitafutia chakula

Kwa Leo tuishie hapo Somo litaendelea..

🇹🇿 MBARIKIWE SANA 🙏
🇹🇿 DOMCITY FARMING CENTER
🇹🇿 17 OCT 2022

AMANI YA MOLA IWE JUU YENU🐓🐓SEHEMU YA KWANZA🐔🐔⛑️⛑️MAKOSA TUNAYOFANYA WAKATI WA KUANZISHA MRADI WA UFUGAJI WA KUKU⛑️⛑️1️⃣...
16/10/2022

AMANI YA MOLA IWE JUU YENU

🐓🐓SEHEMU YA KWANZA🐔🐔

⛑️⛑️MAKOSA TUNAYOFANYA WAKATI WA KUANZISHA MRADI WA UFUGAJI WA KUKU⛑️⛑️

1️⃣ KUANZISHA MRADI WA UFUGAJI USIO KUWA NA MALENGO

👉Watu wengi wamejikuta wakianzisha miradi ya ufugaji bila kuwa na malengo yaani ramani ya kumfikisha kule anapotaka kufika

👉Unakuta mtu ameanzisha mradi wa ufugaji ukimfata na kumuuliza malengo yako ni yepi katika huu mradi wako..??? Hajui atakujibu tu kwa ufupi Mimi napenda kufuga ndio maana nimeanzisha mradi huu

👉Je..?? Hilo jibu linakupa picha gani kwa huyo mtu aliyeanzisha huo mradi...??

📩📩Tunapozungumzia malengo katika ufugaji tunamaanisha nini..?? ili ata wewe unayetaka kuanza mradi au ambaye upo kwenye ufugaji ujue nini Cha kufanya..

📩📩 Mradi wowote lazima uwe na malengo mfano nataka kufuga kuku je malengo yako uuze nini kutoka kwa hao kuku unao Fuga👇👇👇

✍️MAYAI
✍️VIFARANGA
✍️KUKU WAKUBWA(KITOWEO)

📩📩Ukishajua malengo yako ni kuuza kitu gani kati ya hvyo itakupa urahisi ujue nafuga kuku wa aina gani kulingana na malengo uliyojiwekea

💣💣Unakuta mtu anafuga Sasso kwaajili ya kuuza mayai wakati huo Sasso sio wazuri sana kwenye utagaji

📩📩Ukijua malengo yako ni rahisi kufuga aina ya kuku wanaoendana na malengo yako

👉👉Au mtu anamtaji kabsa wa kufuga kuku wa mayai yaani layers ila kwakua hajui unamkuta anapambana na kuku ambao sio watagaji wazuri wa mayai na ukimuuliza anakuambia nawafuga hawa kwaajili ya mayai

🙏🙏Ndugu zangu hapo ndio utakuta mtu anatumia nguvu kubwa mafanikio madogo au akaporomoka kabsa kosa sio wazo alilokua nalo ila changamoto ni namna anavyoendesha mradi wake bila kuwa na mikakati au malengo ya kueleweka

Nazani mpaka hapo umepata picha kidogo somo litaendelea...

🇹🇿 MBARIKIWE SANA 🙏
🇹🇿 DOMCITY FARMING CENTER
🇹🇿16 OCT 22

AMANI YA MOLA IWE JUU YENU🦻🦻80% YA MAGONJWA YA KUKU TUNAYAKINGA KWA CHANJO NA 20% INAYOBAKIA TUNATUMIA DAWA KUWATIBU..👉W...
01/10/2022

AMANI YA MOLA IWE JUU YENU

🦻🦻80% YA MAGONJWA YA KUKU TUNAYAKINGA KWA CHANJO NA 20% INAYOBAKIA TUNATUMIA DAWA KUWATIBU..

👉WAFUGAJI WENGI WAMEKUA WAKIHARIBU CHANJO ZAO BILA WAO KUJIJUA NA KUJIKUTA WANATENGENEZA SUMU BAADA YA KUWAKINGA KUKU WAO

👉KUTOKA NA HILO WAFUGAJI WAMEJIKUTA KATIKA DIMBWI LA MASWALI YASIO NA MAJIBU K**A VILE👇👇👇

🤷BAADA YA KUWAPA CHANJO KUKU WANGU WAMEANZA KUFA..!!

🤷BAADA YA KUWAPA CHANJO KUKU WANGU WAMEANZA KUISHIWA NGUVU ZA MIGUU..!!

🤷KWANINI TUNAWAPA CHANJO HALAFU KUKU WANAKUJA KUUMWA UGONJWA TULIO WAKINGA..!!

🤷NINI UMUHIMU WA KINGA K**A TUNACHOWAKINGA KINAWAUA PIA KUKU WETU..??

🤔🤔HAYO NI BAADHI YA MASWALI WANAYOKUPAMBANA NAYO WAFUGAJI WENGI..??

🔥🔥LEO TUANGALIE NI MAMBO GANI YA KUZINGATIA WAKATI WA UNUNUAJI WA CHANJO, USAFIRISHAJI WA CHANJO,HUIFADHI WA CHANJO NA UTOAJI WA CHANJO
👉ILI CHANJO YETU IWE SALAMA NA YENYE UBORA

✍️Nunua chanjo sehemu rasmi na inayoaminika

✍️Zingatia expired date ya chanjo

✍️Andaa nguvu kazi kulingana na idadi ya kuku wako

✍️Zingatia maelekezo ya chanjo

✍️ Hakikisha uhifadhi bora wa chanjo kutoka dukani hadi shambani

✍️Hauruhusiwi kuhifadhi chanjo kwenye freezer

✍️Hakikisha baada ya kununua chanjo nenda moja kwa moja shambani

✍️K**a hauna elimu ya uchanjaji usiwachanje kuku wako

✍️Usichanganye chanjo na VITAMINI au antibiotics mda wa kuwapa

✍️K**a ulikua unawapa kuku wako antibiotics au dawa hakikisha unasitisha siku mbili kabla ya chanjo

✍️Hakikisha chanjo haipitilizi mda yaani yakitimia masaa mawili toa

✍️Haifai kuchanja kuku wagonjwa

✍️Kuku achomwe sehemu sahihi isiyo na mfupa au mshipa

✍️Baada ya chanjo fukia vitu vyote k**a vile sindano,chupa na mifuko uliyotumia kubebea chanjo

✍️Usitunze sindano kwaajili Cha chanjo ijayo

✍️Chanjo itakayobaki hauruhusiwi kuitunza k**a akiba au kutunza kwaajili ya kumpa mfugaji mwenzako

✍️Hakikisha usafi wa vyombo,nguo na vyote vilivyotumika wakati wa utoaji wa chanjo

✍️Tenganisha kuku waliochanjwa na wasio chanjwa mda wa utoaji wa chanjo

✍️Hakikisha chanjo ya maji mda wa kuifungua mdomo unageukia chini na sio juu

✍️Hakikisha utunzaji mzuri wa kumbukumbu ili ujue tarehe ya chanjo ijayo

🇹🇿 MBARIKIWE SANA 🙏
🇹🇿 DOMCITY FARMING CENTER
🇹🇿 01 OCT 2022

AMANI YA MOLA IWE JUU YENU🇹🇿🌹Kumekua na kawaida ya watu wengi kutumia gharama kubwa kwenye ujenzi wa mabanda ya kuku bil...
23/09/2022

AMANI YA MOLA IWE JUU YENU

🇹🇿🌹Kumekua na kawaida ya watu wengi kutumia gharama kubwa kwenye ujenzi wa mabanda ya kuku bila kujua sifa za banda Bora zinatakiwa kuwa vipi...???

🌹🇹🇿Kuna baadhi ya wafugaji wamejikuta wakipoteza kuku wao kwa magonjwa yasioisha bandani k**a vile mafua n.k bila kujua tatizo limeanzia kwenye ujenzi wa banda lake

🗣️🗣️Ukisoma majalida mbalimbali utakuta maelezo mbalimbali kuhusu sifa za banda Bora la kuku Mimi Leo nitaorodhesha baadhi tu...

👉SIFA ZA BANDA BORA👈
1️⃣BANDA LINATAKIWA LIWE NA UWAZI WA KUTOSHA KURUHUSU HEWA KUINGIA NA KUTOKA
✍️Watu wengi wamekua wakikaririshwa kuwa banda la uwazi sio nzuri eti kwasababu za kuwatesa kuku na baridi na kupelekea wajenge mabanda yenye mfanano na nyumba zetu za kuishi
✍️Narudia tena hii hoja sio sahihi banda la kuku linatakiwa kuwa na uwazi wa kutosha ili kuruhusu mzunguko wa hewa
✍️ Ukijenga banda lako usikariri kwa kuweka uwazi mbele ya banda tu hiyo ni ❌ kosa kwasababu utasababisha hewa chafu mfano yenye vimelea vya magonjwa ikiingia bandani iendelee kuzunguka ndani ya banda na kusababisha maambukizi zaidi kwa kuku wako
✍️Pia kunyima banda kuwa na uwazi wa kutosha ndio chanzo kikubwa Cha magonjwa ya mafua kwa kuku wako
✍️HITIMISHO✍️
Tujenge mabanda yetu kwa kuacha uwazi wa kutosha mbele ya banda na nyuma ya banda ili hewa ikiingia iweze kutoka kiurahisi
🗣️Na wale wanaohofia baridi zipo turubai unaweza zifunga na kuzishusha mda wa jioni au ata wakati wa mvua

2️⃣JENGA BANDA LAKO KWA KUFATA UELEKEO WA JUA NA UPEPO
✍️Siku zote jua linatoka mashariki na kuzama magharibi kwahyo para la banda lako linatakiwa ulijenge kutoka mashariki kuja magharibi ili jua lisimulike ndani ya banda kwa masaa mengi
✍️Alikazalika upepo mara nyingi unaendana na uelekeo wa jua kwahyo ujenzi wako utabaki vilevile banda lianzie mashariki kwenda magharibi

3️⃣JENGA BANDA KWA VIPIMO KULINGANA NA IDADI YA KUKU UNAOTAKA KUWAFUGA
✍️Hili nalo ni jipu kwa wafugaji wengi kwasababu utakuta mtu kajenga banda la kuchukua kuku 100-200 yeye anaweka kuku 500
✍️Vipimo vya banda na idadi ya kuku huwa tunaipata kwa 1M² moja kuchukua kuku wakubwa kuanzia 5-8 hapo itategemea unafuga kuku aina gani chotara wenye maumbo makubwa, layers au kienyeji wenye maumbo madogo..???

SIFA ZIPO NYINGI SANA KWA LEO NAOMBA NIISHIE HAPO KWASABABU SOMO LIKIWA REFU INAWATIA UVIVU WASOMAJI

🌹🇹🇿🌹 MBARIKIWE SANA
🌹🇹🇿🌹 DOMCITY FARMING CENTER
🌹🇹🇿🌹 23 SEP 2022

Address

Dom Town
Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Domcity Farming Center posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category