01/05/2021
NJIA ZA KUONDOA SUMU MWILINI
Sumu ni kitu chochote ambacho kinaweza kuingia mwilini na kusababisha mifumo ya mwili ishindwe kufanya kazi ipasavyo.
Unaweza ukawa unafikiria kuwa una afya njema, lakini haujisikii vyema n abado unaendelea kupuuzia na kudhani ni hali ya kawaida hapana hakuna jambo dogo kwenye Afya ya mtu kwa hivyo ni vyema kushuulikia afya na hali yako kwa kwenda hospitali au kuonana na wataalam wa afya kwa ajili ya uchunguzi zaidi na matibabu.
Usingoje mpaka tatizo likawa kubwa na hatimaye unafika hospitali kwa uchunguzi hapo ulishazidiwa sana na kuambiwa kwamba unasaratani au figo zimefeli hapo ndio utakapopata mshtuko mkubwa zaidi na pressure huanzia hapo na furaha ya maisha yako pia huanza kutoweka. Na bado hapohapo hawatoweza kukupa sababu au chanzo cha huo ugonjwa zaidi ya kukueleza kuwa chakula na mtindo wa maisha uliokuwa unaishi kwa ujumla ndio sababu kubwa.
Na madhara kiujumla ni mengi mno sio tu figo na saratani bali hata kukosa choo, kiungulia, vidonda vya tumbo, ini kuharibika, ugonjwa wa moyo, sukari , pressure vyote vinaweza vikawa vinakunyemelea au kukupata.
Napo sema maisha uliokuwa ukiishi yanaweza kua yamechangia namaanisha Aina za vyakula ulivyokuwa ukivila ambavyo haviwezi kukujengea mwili wala kukukinga na maradhi, na nikisema sumu mwilini simaanishi sumu za kuwekewa au kung'atwa na nyoka au wadudu hapana nasemea sumu zinazoingia kwenye mwili wa binadam na kuanza kuleta madhara taratibu taratibu. Nitajaribu kuzielezea hapo chini kwa ufupi tu ili upate upate picha halisi.
Ndugu yangu naomba uelewe tu hili mapema kwamba Kinga ni Bora kuliko Tiba. Mana kuna maradhi mengine unaweza kuyakinga lakini huwezi kuyapatia Tiba.
Magonjwa k**a Saratani, Sukari kupata tiba yake ni mtihani mkubwa labda unaweza ukatuliza kwa muda na sio kupata uponyaji wa moja kwa moja.
Haileti furaha kila kukicha tupo kwenye milango ya madaktari, kwa sababu hata dawa pia tukitumia kwa muda mrefu zinakuwa sio nzuri kwa fya zetu. Kila kukicha Afya za watu zinazidi kuzorota na hii inasababishwa na aina za vyakula vyetu tunavyotumia. Embu jiulize mbona wazee wetu wa zamani afya zao hazikuwa k**a za kizazi cha sasa?
AINA ZA SUMU ZINAZODHOOFISHA AZYA ZETU NI K**A:-
1) Ni sumu tunazozivuta katika hewa kila siku kutokana na mioshi ya magari, viwanda n.k. Ni lazima tuvute hewa ya oxygen ili tupate kupumua na kusihi lakini hewa yenyewe tunayovuta inakuwa si hewa salama na asilimia kubwa imetanda kila sehem kutokana na maendeleo
2) Matumizi ya pombe na uvutaji wa sigara kupita kiasi
3) Sumu zinazotokana na matumizi ya dawa mbalimbali tunayotumia kutibu afya zetu, sumu zinazotokana na matumizi ya vidozi mbalimbali tunavyotumia kwa ajili ya urembo na kupendeza.
MAJANGA YOTE HAYO HAYADHURU AFYA ZA BINADAMU KWA MARAMOJA HUTOKEA TARATIBU HATA KWA MIAKA NA MIAKA LAKINI HUUA KWA ASILIMIA KUBWA ZAIDI
Tunaingiza sumu nyingi mwilini kw anjia ya vyakula, vinywaji, hewa , amatumizi ya vipodozi. Vyakula vingi tunavyokula sio salama sana, vipodozi vingi vimehejaa kemikali hatarishi kwa afya zetu yani hatuna pa kukwepea, njia sahihi iliyobaki ni kujitahidi kupunguza madhara ya sumu ziingiazo mwilini kwa njia hizo za uvutaji hela, ulaji wa vya kula, matumizi ya vipodozi vyenye kemikali na hata utumiaji wa vinywaji vyenye madhara mwilini au MATUMIZI YA VIRUTUBISHO KWA WINGI ndio vinaweza vikaokoa jahazi.
Dalili hizi ni ishara ya mwili wako kuwa umebeba sumu mwilini:
1. Uchovu sugu
2. Maumivu ya maungio
3. Msongamano puani
4. Kuumwa kichwa kila mara
5. Tumbo kujaa gesi
6. Kufunga choo au kupata choo kigumu
7. Kukosa utulivu
8. Matatizo mbalimbali ya ngozi ikiwemo chunusi
9. Pumzi mbaya
10. Mzunguko wa hedhi usio sawa
11. Kuishiwa nguvu
12. Kushindwa kupungua uzito
13. Kupenda kula kula kila mara
14. Kupatwa na ganzi sehemu mbalimbali mwilini
Mwili huzalisha sumu hizi kila wakati unapofanyika mmeng'enyo au usagaji wa chakula katika mwili wako.
NJIA ZA KUONDOA SUMU MWILINI
1)Ulaji wa matunda na mbogamboga
2)Pendelea kula vyakula asilia, punguza au acha kula vyakula vya viwandani k**a vile vya makopo, fast food au vya dukani (Chips, burger nk) havina msaada kwa afya yako
3)Jitahidi unywe maji mengi kwa siku yani mara kwa mara. Kwa mtu mzima sio chini ya litre tatu au unywe angalau glass 8 mpaka 10 kwa siku. Maji husaidia kuflash sumu mwilini mana asilimia kubwa ya mwili ni maji hivyo yanakazi kubwa katika afya yako
4)Punguza au acha kabisa kunywa vinjwaji vyenye caffeini hasa chai ya kutumia majani ya chai pamoja na kahawa
5)Jitahidi upate masaa 8 ya kulala kwa siku ili kuupumzisha mwili na kujenga afya yako zaidi
6)Kwa usalama wa afya yako jitahidi ukae maeneo enye viwanda vingi na migodi
7)Kula vyakula ambavyo havijakpobolewa kwa wing k**a brown bread nk
8) Kaa mbali na mambo ambayo yanaweza kukuletea stress mana asilimia kubwa ya magonjwa huletwa na stress kwa mfano pressure, ugonjwa wa moyo nk watu wengi zaidi huchagua kunywa vilevi mara baada ya kujiskia stress wakidhani wanajiokoa kumbe ndio kwanza wanaongeza ukubwa wa tatizo
9)Epuka unywaji holela wa dawa za hospitali (kizungu) na hata utumiaji uliopita kipimo wa dawa za asili. Mana vyote vikizidi hudidimiza afya ya mtumiaji na kumletea maradhi mengine ambayo hakuyategemea k**a figo kufeli, ini nk
10)Matumizi yaliyopita kiasi ya vilevi k**a bia, gongo na pombe , madawa ya kulevya, bangi na vinginevyo ni vitu vinavyopelekea mwili kuwa na taka moja kwa moja.
Namna pekee ya kuondoa sumu kutokana na vilevi ni kuviacha kabisa hivyo vilevi.
DAWA YA KUTOA SUMU MWILINI >>Aloevera Gel Juice
Inasaidia mwili wa binadamu kupambana na matatizo mbalimbali katika mwili k**a > Kuboresha mmeng'enyo wa chakula>Inapunguza Acid Tumboni>Kuondoa SUMU/TAKA MWILI zitokanazo na vyakula, madawa, Pombe, Sigara nk > Kurutubisha Ngozi kwa kuondoa CELL zilizokufa na kutengeneza upya >Kuondoa msongo wa mawazo (stress) > Huimarisha mfumo wa damu na kuondoa mafuta yasiyohitajika >Kuuongezea mwili nguvu na kinga zaidi > Kusafisha utumbo mpana na kusaidia kupata choo vizuri.
Inaamino Acid nyingi zaidi ya 18 ambazo 7 kati ya hizo ni muhimu sana katika ukuwaji wa chembechembe za uhai katika mwili wa binadamu.
Angalizo:
Hata ukichanganga mboga zote pamoja na matunda bado hayatafikia virutubisho vilivyopo kwenye aloevera gel juice.
Tahadhari: Sio Aloevera zote zinakuwa zinafaa katika mwili wako nyingine ni sumu kwa binadamu. Kuna aina karibia 300 za mmea huu lakini mpaka sasa iliyothibitika kwamba ni salama kwa mwili wa binadamu ni aina moja tuu. Kuwa makini katika hilo.
Usitumie dawa hii bila maelekezo ya mtaalam.
K**a utahitaji maelezo zaidi ya jinsi ya jinsi ya kutumia juice hii k**a tiba ya asili na upatikanaje wake
Wasiliana nami
Msambazaji/Wakala: Bunyige Vincent
0742314037/0769313380
Tafadhali SHARE post hii kwa ajili ya wengine uwapendao.