01/01/2026
Heri ya Mwaka Mpya 2026
Mwaka jana 2025 nilisema nitaongelea *Kwa nini tufanye Biashara Moja tu hata k**a tuna uwezo wa kuanzisha zaidi ya moja?*
Hizi hapa ndio sababu zenyewe:-
Kumbuka kwenye somo la kwanza la mwaka jana 2025 tuliangazia ni Biashara ipi unapaswa ufanye na tukasema ni ile unayoipenda na kuijua vizuri.
Kwa kuzingatia hilo leo ni mwendelezo kwenye hili somo la pili.
Sababu ya kwanza ya kuepuka kuwa na Biashara zaidi ya moja:
1.Kuwa na muda wa kutosha kuisimamia biashara hiyo.
Maana biashara unapoianzisha inahitaji mwanzilishi awe karibu sana k**a mtoto mdogo anavokuwa karibu na mama yake pindi anapozaliwa, kadiri unavyozidi kukua ndio uboreshaji wa mifumo ya uendeshaji huhitajika.
Ukianzisha zaidi ya moja ni dhahiri umejipanga kufeli au kuchelewa kukua kwenye Biashara.
Kuwa na Biashara zaidi ya moja hii ni hatua ya pili baada ya hatua hii ya kwanza *kufanikiwa.*
Biashara kufanikiwa ni nini?
Biashara inakuwa haikuhitaji wewe uwepo ndio itoe huduma, haihitaji hela za mfukoni kwako ndio iende.
Hapo ndipo Biashara zingine za ya moja huzaliwa maana utakuwa unaanzisha kwa lengo la kusapoti huduma au biashara mama na hapo hapo nayo inakuwa inaingiza pesa.
Mfano:Una biashara ya mazao, biashara ikafanikiwa ukaamua ununue Lori ili iwe rahisi kuwahudumia wateja wako,hapo hapo utapanga mfumo wa kuhudumia wengine na kuanza kupata hela nyingine.
Ongezea zingine
2.
3.
Kwa upande wangu kabla sijaanza kufanya biashara nilisoma vitabu mbalimbali na kukutana na wengi kwenye biashara na wote ili kuwa ni kuanzisha biashara moja na si zaidi ila niliona wananitania,nikaona wananichelewesha kuwa na hela, maana hela ninayo ya kuanzisha biashara zaidi ya moja kwa nini nisifanye?
Niliamua kuiacha kanuni na kutengeneza kanuni yangu ya kuvuna mihela mingi na jibu hela nilizizika na kubakiwa na biashara moja.
Saivi nafata masharti naendelea vizuri,sasa na wewe mpendwa wa Mungu usije ukakaidi ukapata hasara.
*Somo la tatu litakuwa kwa nini hupaswi kuanza na mtaji mkubwa sana na ba